Michuano ya UEFA Champions League inaendelea tena leo kwa michezo sita ya kusisimua, huku baadhi ya vigogo barani Ulaya wakishuka dimbani kutafuta ushindi na pointi muhimu.
Mchezo wa kwanza utapigwa saa 1:45 usiku, ambapo Barcelona itakuwa mwenyeji wa Feyenoord, kabla ya michezo mingine minne kuanza saa 4:00 usiku.
Miongoni mwa mechi zinazotarajiwa kupewa attention kubwa ni Liverpool vs Atletico Madrid, mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa timu zote mbili.
Pia kuna Napoli vs Arsenal, pambano jingine la kibabe ambalo linatarajiwa kuvuta macho ya mashabiki wa soka, huku Arsenal ikitafuta matokeo muhimu dhidi ya Napoli.
Kwa ujumla, ni usiku mwingine wa soka la kiwango cha juu kwenye UEFA Champions League, na mashabiki watapata burudani kutoka mwanzo hadi mwisho.