Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama, amesema mambo yanayoendelea nje ya uwanja kuhusu yeye si sehemu ya maisha anayoyahusudu na wala hayamkatishi tamaa katika kuendelea na majukumu yake ya soka.
Chama ameyasema hayo leo wakati wa tukio la Media Day lililofanyika katika Uwanja wa MO Arena, Bunju jijini Dar es Salaam, huku kauli yake ikija wakati ambapo kumekuwa na mjadala kuhusu uhusiano wake na klabu yake ya zamani, Yanga SC.
Nyota huyo wa Zambia amesisitiza kuwa anachagua kuendelea kuzingatia maisha yake ya soka na majukumu yake ndani ya Simba, badala ya kuathiriwa na mambo yanayoendelea nje ya uwanja.