Local, Transfer News, Washington Spirit, Al-Nassr, Yanga

Clara Luvanga aweka historia Marekani, asajiliwa kwa rekodi Tanzania

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2h ago
Clara Luvanga aweka historia Marekani, asajiliwa kwa rekodi Tanzania

Mchezaji wa Kimataifa wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Clara Luvanga, ameandika historia mpya katika soka la wanawake baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Al-Nassr ya Saudi Arabia kwenda Washington Spirit ya Marekani.

Luvanga amesaini mkataba wa miaka minne utakaomuweka Washington Spirit hadi mwaka 2029, katika usajili unaoelezwa kuwa na thamani ya takribani dola milioni 2.3(zaidi ya Tsh 6B)

Kiasi hicho kinatajwa kuwa ada kubwa zaidi ya uhamisho kuwahi kulipwa kwa mchezaji wa soka la wanawake, hivyo kumweka Luvanga katika ukurasa mpya wa historia ya soka la wanawake duniani.

Rekodi mpya kwa Tanzania

Uhamisho huo pia unampa Luvanga heshima ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika historia ya National Women’s Soccer League (NWSL) nchini Marekani.

Hatua hiyo ni mafanikio makubwa kwa Luvanga binafsi na Tanzania kwa ujumla, huku akizidi kuiweka nchi kwenye ramani ya soka la wanawake duniani.

Safari ya Luvanga imekuwa ya kuvutia, kuanzia Yanga Princess, akipiga hatua hadi soka la Hispania, kisha kujiunga na Al-Nassr nchini Saudi Arabia na sasa kuhamia Marekani.

More Stories

Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga
Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga
2h ago
READ MORE β†’
Kimoto akalia kuti kavu baada ya kipigo dhidi ya Mashujaa Fc
Kimoto akalia kuti kavu baada ya kipigo dhidi ya Mashujaa Fc
2h ago
READ MORE β†’
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
6h ago
READ MORE β†’
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
7h ago
READ MORE β†’
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
7h ago
READ MORE β†’
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
8h ago
READ MORE β†’
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
9h ago
READ MORE β†’
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
10h ago
READ MORE β†’
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
10h ago
READ MORE β†’