Mshambuliaji wa Chelsea, João Pedro, ametangazwa rasmi kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi wa Agosti katika Premier League.
João Pedro ameanza vyema msimu akiwa na Chelsea, akihusika katika mabao manne ndani ya mechi tatu, akifunga mabao mawili na kutoa assists mbili.
Kiwango hicho kizuri mwanzoni mwa msimu kimemfanya pia kurejea kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Brazil.