Local, Normal News, CAFCL, Yanga, Gaborone United

Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United

Joel JJ By Joel JJ
27m ago
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United

Kocha Mkuu wa Gaborone United, Sean Connor, ameweka wazi kuwa timu yake haitaingia kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya Yanga ikiwa na hofu, akiamini presha kubwa zaidi ipo upande wa wenyeji watakaokuwa wakicheza mbele ya mashabiki wao.

Gaborone United inatarajiwa kushuka dimbani Jumamosi kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam, katika mchezo wa marudiano wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Baada ya matokeo ya sare ya bao 1-1 mchezo wa kwanza, Connor amesema anatambua ukubwa wa kazi iliyo mbele yao, lakini anaamini kikosi chake kina uwezo wa kuipa Yanga wakati mgumu na kutafuta matokeo yatakayowasaidia kusonga mbele.

Kocha huyo amesema Yanga inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na mzigo mkubwa wa matarajio kutokana na kucheza nyumbani, huku mashabiki, vyombo vya habari na mazingira ya klabu yakiongeza presha kwa wenyeji.

Amesema Gaborone United inataka kuitumia hali hiyo kama nafasi ya kucheza bila mzigo mkubwa na kuilazimisha Yanga kufanya makosa.

Licha ya kuiona presha ikiwa upande wa Yanga, Connor hajaficha heshima yake kwa kikosi cha Wananchi.

Amesema wameutambua ubora wa Yanga, akitaja uwezo wa wachezaji wake, kasi yao pamoja na mchango wa benchi la ufundi kama mambo ambayo Gaborone United italazimika kuyadhibiti.

More Stories

Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
2h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
4h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
5h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
5h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
7h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
10h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
17h ago
READ MORE →
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
23h ago
READ MORE →
Rasmi: Hemed Suleiman “Morocco” ametangazwa kocha mpya wa TRA United
Rasmi: Hemed Suleiman “Morocco” ametangazwa kocha mpya wa TRA United
23h ago
READ MORE →