TRA United wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa NBC Premier League, matokeo ambayo yamevunja ukame wao wa ushindi baada ya kupitia michezo tisa mfululizo bila kushinda.
Ushindi huo umekuja katika wakati muhimu kwa TRA United, ambao walikuwa wakihitaji matokeo chanya ili kurejesha morali ya timu baada ya mwenendo usioridhisha katika michezo yao ya nyuma.
Huu pia ni ushindi wa kwanza wa TRA United chini ya kocha mpya Hemed Suleiman “Morocco”, ambaye ameingia kwenye benchi la timu hiyo akiwa na siku tatu pekee tangu kutangazwa rasmi kuwa kocha mpya.
Licha ya muda mfupi wa kufanya kazi na kikosi, Hemed Suleiman ameanza kwa matokeo mazuri, akiongoza TRA United kuondoka ugenini na pointi zote tatu. Ushindi huu unaweza kuwa mwanzo wa mabadiliko katika mwenendo wa timu hiyo kuelekea michezo ijayo ya NBC Premier League.
FT: Pamba Jiji 1-3 TRA United.
TRA United wameanza ukurasa mpya chini ya “Morocco” kwa ushindi muhimu.