Kwa sasa nchini Tanzania, ukiachana na Pacome Zouzoua, ambaye yupo nje ya uwanja kutokana na majeraha, Libasse Gueye anaonekana kuwa miongoni mwa mawinga hatari na machachari zaidi kwenye soka la Tanzania.
Gueye si mchezaji anayehusika na kutengeneza nafasi pekee, bali ana uwezo mkubwa wa kutoa assist pamoja na kufunga mabao, jambo linalomfanya kuwa tishio la muda wote kwa safu za ulinzi za wapinzani.
Mwinga huyo amekuwa akionyesha uwezo wa kutumia kasi, ujanja na ubunifu wake kuvuruga mipango ya mabeki, huku uwezo wake wa kucheza katika maeneo tofauti ya safu ya ushambuliaji ukimpa thamani zaidi kwenye kikosi.
Kwa upande wa Simba SC, Gueye amekuwa miongoni mwa wachezaji muhimu na tegemezi katika kikosi.
Uwepo wake umeendelea kuwa na mchango mkubwa katika namna Simba inavyoshambulia na kutengeneza nafasi za kufunga.
Mara kadhaa imeonekana kwamba pale Gueye anapokosekana kwenye mchezo, Simba hupata changamoto zaidi katika kutengeneza nafasi, kuongeza kasi kwenye mashambulizi na kupata matokeo mazuri.
Hali hiyo inaonyesha umuhimu wake ndani ya kikosi na kwa nini wapinzani wamekuwa wakihitaji kuwa makini zaidi wanapokutana na Simba akiwa kwenye kiwango chake.
Kwa uwezo wake wa kufunga, kutoa assist na kuvuruga safu za ulinzi, Libasse Gueye anaendelea kujitengenezea nafasi miongoni mwa mawinga wanaohitaji uangalizi mkubwa kwenye soka la Tanzania kwa sasa.