Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Shaban Kamwe, amethibitisha kuwa mshambuliaji wa timu hiyo, raia wa Namibia Peter Shalulile, amepata jeraha baada ya kuumia katika mchezo wa CAF Champions League dhidi ya Gaborone United.
Shalulile amekuwa miongoni mwa wachezaji muhimu wa Yanga ambapo dhidi ya Gaborone United, alifunga bao moja lililosaidia timu hiyo kuvuka hatua ya kwanza ya mashindano kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2. Katika mchezo wa marudiano.
Hali ya nyota huyo bado haijakaa sawa kwa mujibu wa meneja habari wa timu hiyo ikiwa ni kuelekea mchezo wa ligi kuu bara utakaochezwa hii leo majira ya saa 1 usiku dhidi ya Geita gold
Yanga inashuka uwanjani hii leo kwenye muendelezo wa ligi kuu bara katika uwanja wa kmc uliopo mwenge jijini Dar es salaam