Local, Normal News, Simba, Barker, Azam, Azam complex, Ligi kuu bara

Ushindi dhidi ya Azam ni muhimu kwa malengo ya simba: Steve Barker

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
22h ago
Ushindi dhidi ya Azam ni muhimu kwa malengo ya simba: Steve Barker

Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema ushindi dhidi ya Azam FC ni muhimu kwa timu hiyo katika safari yake ya kuwania malengo ya msimu huu, huku akikiri kuwa maandalizi ya mchezo huo yamefanyika ndani ya muda mfupi.

Barker amesema Simba haikuwa na muda mrefu wa kujiandaa baada ya mchezo wao wa mwisho, lakini hilo halipunguzi umuhimu wa kupata matokeo mazuri dhidi ya Azam FC. “Tulikuwa na muda mchache wa maandalizi tangu kucheza mchezo wa mwisho, ila mechi hii ni muhimu kwetu kupata ushindi ili kufikia malengo yetu ya msimu huu,” alisema Barker.

Kocha huyo ameongeza kuwa Simba inalenga kubadilisha matokeo ya msimu uliopita dhidi ya Azam, ambapo ilipoteza jumla ya pointi nne katika michezo yao miwili ya Ligi Kuu. Barker amesema msimu huu wanataka kufanya vizuri zaidi katika michezo dhidi ya wapinzani wao hao.

Mchezo huo wa raundi ya sita ya NBC Premier League umepangwa kuzikutanisha Azam FC na Simba SC katika Uwanja wa Azam Complex. Simba inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na rekodi nzuri ya kuanza msimu, huku Azam ikiwa miongoni mwa timu zinazoshindania nafasi za juu.

More Stories

Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
25m ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
1h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
1h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
14h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
15h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
16h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
20h ago
READ MORE β†’
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
20h ago
READ MORE β†’
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
21h ago
READ MORE β†’