Local, Normal News, AFCON 2027, Africa, Tanzania, Zanzibar,

Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu
β€’
1h ago
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027

Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Dk. Patrice Motsepe, anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kesho, Septemba 17, 2026, kwa ziara inayolenga kukagua maendeleo ya maandalizi ya AFCON 2027.

Katika ziara hiyo, Motsepe ataungana na maofisa mbalimbali wa CAF kufanya ukaguzi wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, pamoja na kutathmini hatua zilizofikiwa katika maandalizi ya mashindano hayo yatakayofanyika Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa TFF, Motsepe pia anatarajiwa kukutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi ya AFCON 2027, Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, pamoja na viongozi wengine wanaohusika na maandalizi ya mashindano hayo.

Katika ziara yake, Rais huyo wa CAF atakagua maeneo mbalimbali ya Uwanja wa Benjamin Mkapa ili kufuatilia maendeleo ya miundombinu na kuhakikisha maandalizi yanaendelea kwa kuzingatia mahitaji ya mashindano ya AFCON 2027.

Motsepe atakuwa ameambatana na viongozi kadhaa kutoka CAF na CECAFA, akiwemo Kurt Okraku, Feizal Sidat, Paulos Andemariam Weldehaimanot na Samson Adamu.

Ziara hiyo inatajwa kuwa sehemu muhimu ya ufuatiliaji wa maandalizi ya Tanzania kuelekea AFCON 2027, huku nchi ikiwa miongoni mwa wenyeji wa mashindano hayo.

More Stories

Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
28m ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
1h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
14h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
15h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
16h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
20h ago
READ MORE β†’
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
20h ago
READ MORE β†’
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
21h ago
READ MORE β†’
Ushindi dhidi ya Azam ni muhimu kwa malengo ya simba: Steve Barker
Ushindi dhidi ya Azam ni muhimu kwa malengo ya simba: Steve Barker
22h ago
READ MORE β†’