Manchester United imetupwa nje ya EFL Cup baada ya kufungwa 3-2 na Brighton & Hove Albion katika mchezo wa raundi ya tatu uliochezwa Old Trafford.
United ilianza kwa kasi kubwa, ikifunga mabao mawili ndani ya dakika 10 kupitia Shea Lacey dakika ya 8 na Mason Mount dakika ya 10, lakini Brighton haikukata tamaa.
Charalampos Kostoulas alipunguza bao kabla ya mapumziko, kisha Pascal Groß akasawazisha dakika ya 65. Dakika nne baadaye, Maxim De Cuyper akaikamilisha comeback ya Brighton kwa bao la tatu. (Sky Sports)
Matokeo hayo yanaifanya Manchester United kuaga EFL Cup katika hatua ya tatu, huku Brighton ikifuzu kwenda hatua ya 16 bora.
Kwa United, mwanzo wa msimu unaendelea kuwa mgumu: imepata pointi 4 kati ya 12 katika Premier League na sasa imetolewa pia kwenye EFL Cup.