Wakat Ligi Kuu ya NBC ikisimama kwa takribani wiki tatu kupisha kalenda ya FIFA, ni mafahari wawili pekee Yanga na Simba ambao wamegoma kupoteza mchezo mpaka sasa.
Timu hizo zimefungua mapema ushindani kwenye mbio za ubingwa zikibanana kwenye alama 18 baada ya kushinda mechi sita.
Yanga imeendelea kusalia kileleni kutokana na faida ya uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa (+14) huku Simba ikiwa na (+9).
Azam Fc iliondoka kwenye orodha ya timu ambazo hazijapoteza mchezo msimu huu baada ya kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Simba hapo jana.
Kipigo hicho pia kiliivurugia Azam Fc rekodi ya kutopoteza mchezo kwenye uwanja wake wa nyumbani katika msimu wa pili mfululizo.

