Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wameingia kambini jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya mechi mbili za kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).
Taifa Stars inajiandaa kukutana na Guinea-Bissau katika mchezo wa kwanza wa kampeni hiyo, utakaopigwa Septemba 25, 2026, kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Baada ya mchezo huo, Stars itasafiri kwa ajili ya kukutana na Madagascar katika mchezo wa pili wa kufuzu AFCON 2027, utakaochezwa ugenini Septemba 29, 2026.
Kuingia kwa wachezaji kambini kunaashiria mwanzo wa maandalizi ya kikosi kuelekea michezo hiyo miwili ambayo itakuwa sehemu ya safari ya Tanzania katika kujiandaa na fainali za AFCON 2027.
Tanzania ni mmoja wa wenyeji wa michuano hiyo ya PAMOJA na Kenya na Uganda. Wanashiriki hatua ya kufuzu kwa mujibu wa kanuni tu na kama sehemu ya maandalizi ya kuelekea michuano hiyo kwani tayari tiketi wanayo.



