Local, Normal News, Ligi kuu bara, Geita Gold, Yanga, Aziz KI, TFF

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
2h ago
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya

Beki wa Geita Gold FC, Datius Peter, amesema tukio la kuchezewa rafu na kiungo wa Yanga SC, Stephane Aziz Ki, lilikuwa la bahati mbaya na si kitendo cha makusudi, huku akieleza kuwa anaendelea vizuri baada ya kupata maumivu katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Septemba 15, 2026.

Datius aliumia baada ya Aziz Ki kumchezea faulo katika dakika za mwanzo za mchezo kati ya Geita Gold na Yanga kwenye Uwanja wa KMC Complex. Akizungumza baada ya mchezo huo, Datius alisema Aziz Ki hajawahi kuwa na rekodi ya kucheza madhambi ya aina hiyo, akiamini mguu wa kiungo huyo ulikuwa ukijaribu kukinga mpira.

“Aziz KI hajawahi kucheza rafu kama hizo, nafikiri ilikuwa bahati mbaya kwakuwa mguu wake ulitaka kukinga mpira sasa uwepesi wangu uwanjani ndio ikatokea hivyo,” alisema Datius, akieleza kuwa kwa sasa anaendelea vizuri na ameanza mazoezi.

Katika tukio hilo, mwamuzi Abdisalam Wajih alimwonyesha Aziz Ki kadi ya njano awali, kabla ya kwenda kwenye mfumo wa VAR na kubadilisha uamuzi huo kwa kumpa kadi nyekundu ya moja kwa moja. Yanga ilicheza ikiwa pungufu kwa zaidi ya dakika 70, lakini ikafanikiwa kushinda 1-0 kupitia bao la Farouk Koumara.

Datius amesema baada ya tukio hilo alibainika kuwa na uvimbe katika eneo la enka na sehemu ya juu ya ugoko, lakini matibabu aliyopata yamesaidia hali yake kuimarika.

More Stories

LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
3h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
6h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
6h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
7h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
7h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
15h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
19h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
20h ago
READ MORE β†’