Leseni yamkwamisha Katwila Ihefu Fc

Joel JJ By Joel JJ • 17th February 2023


Leseni yamkwamisha Katwila Ihefu Fc

Katibu Mkuu wa Ihefu, Zagalo Chalamila amesema uamuzi wa timu hiyo kumtangaza kocha mkongwe John Simkoko kuwa Kocha Mkuu umetokana na  kocha wao Zubery Katwila kukosa sifa za kukaa kwenye benchi

Zagalo amesema baada ya kuondoka kwa Juma Mwambusi walipewa nafasi ya Katwila kuongoza kati ya michezo minne hadi mitano, na baada ya hapo walitakiwa kutafuta kocha mwenye vigezo vinavyotakiwa.

"Wengi wanadhani Katwila hatumuamini, lakini wanashindwa kuelewa ana leseni 'B' na ili ukae katika benchi unatakiwa uwe na 'A' ya CAF, ndiyo maana unaona amerudi darasani kusoma," alisema

Zagalo alisema wana matumaini makubwa na ushirikiano uliopo baina ya Katwila na Simkoko huku akiweka wazi uzoefu wake utakuwa na manufaa makubwa katika kikosi chao ambacho kimekuwa na matokeo mazuri kwa sasa.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.