Makamu wa Rais wa Yanga Arafat Haji amesema matunda yanayoonekana sasa ni matokeo ya uwekezaji mkubwa uliofanyika ndani ya klabu hiyo
Arafat amesema wamefanya usajili wa wachezaji bora na benchi la ufundi lililosheheni watu mahiri wakiongozwa na Profesa Nasreddine Nabi ambaye tetesi zimeanza juu ya kuhitajika kwake na vigogo wa soka barani Afrika hasa baada ya kuiongoza Yanga kutinga robo fainali kombe la Shirikisho barani Afrika
Arafat amesema klabu ina malengo ya muda mrefu hivyo haitakubali kocha wake aondoke kirahisi
"Kitu pekee ambacho kinatutofautisha na wapinzani wetu wengi ni kuwa na benchi la ufundi pana lenye wataalam bora"
"Nabi kuondoka linawezekana lakini haiwezi kuwa sasa, nadhani hata yeye anaamini yuko katika klabu ambayo hatua chache zijazo anaweza kuwa katika rekodi kubwa zaidi ya mafanikio," alisema Arafat
"Bado tunamhitaji sana Nabi niwahakikishie mashabiki wetu kwamba kocha wao huyu na mwingine haitakuwa rahisi kwetu kuwaachia, tuna malengo makubwa na hii ni safari tu ya kufika huko"
"Tunafahamu hizi taarifa za sisi kuwa na kocha bora kama Nabi wengine ni ndoto zao, Yanga tuko katika mafanikio haya kutokana na kutumia nguvu kuwaweka wataalam wote bora kama hawa, utulivu wa namna hii klabu zingine hazina ndio maana wanayumba kila wakati"



