Waamuzi waliomaliza adhabu wabaki katika uangalizi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th March 2023


Waamuzi waliomaliza adhabu wabaki katika uangalizi

Licha ya baadhi ya waamuzi kumaliza adhabu zao za kufungiwa, Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Nassor Hamduni amesema wataendelea kuwa chini ya uangalizi maalumu hadi pale watakapojiridhisha

Hamduni alikiri kuwepo kwa waamuzi ambao wamemaliza adhabu walizopewa lakini amesisitiza kwa sasa kuwaweka kwenye ratiba ni mapema hadi pale watakapoona inafaa kuwarejesha.

Mmoja ya waamuzi ambao wamemaliza adhabu ni pamoja na Ahmed Arajiga ambaye alifungiwa miezi sita kutokana na makosa mbalimbali ya kujirudia katika kutafsiri sheria za soka uwanjani

"Bado hatujawarejesha hadi sasa ili tuone namna gani tutafanya hivyo, wanaweza wakarejea uwanjani kama ambavyo nia yetu ilivyo lakini wanaweza wakaonekana msimu ujao"

"Kwa sasa siwezi kufanya tathmini ya kiwango cha waamuzi kama kimeongezeka au kimepungua lakini msimu ukimalizika naweza kufanya hivyo kwa kuangalia ripoti mbalimbali," alisema Hamduni.

Hata hivyo, aliongeza kuna baadhi wamesharudishwa ndio maana kunaonekana kuna ubora katika michezo ya ligi mbalimbali zinazoendelea tofauti na hali ilivyokuwa siku za nyuma.

"Arajiga licha ya kumaliza miezi sita lakini yupo katika uangalizi kama ilivyo kwa kina, Sasii (Elly) na wengine, hivyo tunaomba wadau watuvumilie kidogo," Hamduni alinukuliwa na gazeti la Mwanaspoti


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.