Lionel Messi aliongeza rekodi mpya kwenye wasifu wake siku ya Jumamosi, akiwa mfungaji bora katika historia ya ligi kuu tano bora barani Ulaya
Kwa bao alilofunga Jumamosi dhidi ya Lens, Muargentina huyo wa PSG anafikisha mabao 495 sawa na Cristiano Ronaldo kabla ya kuondoka kwenda Saudi Arabia
Bao hilo (la 15 kwenye Ligue 1) linamfanya Messi kufikisha 21 katika misimu yake miwili kwenye Ligue 1, huku akifunga 474 kwenye LaLiga Santander akiwa na Barcelona.
Kwa upande wake, Cristiano mabao hayo 495 yamegawanywa kama ifuatavyo: 84 akiwa Manchester United; 311 akiwa Real Madrid; 81 akiwa Juventus; na 19 katika awamu yake ya pili United
Wiki moja kabla, Messi pia alikua mfungaji bora wa muda wote katika ngazi ya klabu barani Ulaya akiwa na mabao 702.
Sasa, akiwa na bao lake la hivi karibuni, ana mabao 703 katika mashindano yote katika ngazi ya klabu barani Ulaya. Cristiano, barani Ulaya, alifunga mabao 701 katika mashindano yote.



