Aubameyang agusa mpira mara 9 Chelsea ikipigwa 3-1 na Arsenal

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd May 2023


Aubameyang agusa mpira mara 9 Chelsea ikipigwa 3-1 na Arsenal

Ulikuwa usiku wa mateso kwa Chelsea huko Emirates mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang akianza dhidi ya waajiri wake wa zamani katika mchezo ambao Frank Lampard alimtumia kwa dakika 45 tu huku akigusa mpira mara tisa

Fowadi huyo, ambaye aliwakilisha The Gunners kwa miaka minne, alishuhudia Chelsea ikikubali kichapo cha 3-1 kwenye Uwanja wa Emirates Jumanne usiku

Lakini Chelsea walikuwa wa pili kwa ubora katika kila idara kwani waliruhusu mabao 3-0 ndani ya dakika 34 za mwanzo

Martin Odegaard aliweka The Gunners mbele dakika ya 18 akiunganisha krosi kutoka kwa Granit Xhaka upande wa kushoto kabla ya kupiga shuti lililopita Kepa Arrizabalaga

Wawili hao walishirikiana tena baada ya nusu saa baada ya Xhaka kuwa mtoa huduma kwa Odegaard, ambaye alifunga bao lake la pili na la Arsenal kwa kumaliza pasi murua

Na muda mfupi baada ya hapo ikawa 3-0 pale Gabriel Jesus alipoweka mpira mbele ya Kepa kutoka karibu na eneo la hatari baada ya makosa ya safu ya ulinzi ya Chelsea

Noni Madueke alifunga bao la ugenini kipindi cha pili lakini haikuwa faraja kwa Chelsea usiku wa kuamkia leo. Ilikuwa mchezo mbaya kwa wachezaji wa Frank Lampard lakini Aubameyang alikuwa na wakati mbaya zaidi akigusa mpira mara tisa tu katika kipindi cha kwanza

Arsenal imerejea kileleni mwa msimamo ikifikisha alama 78, alama mbili zaidi ya Manchester City inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 76

Hata hivyo Manchester City wana mechi mbili mkononi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.