Kocha Mkuu wa Ruvu Shooting Mbwana Makata alisema hawajakata tamaa na wanaendelea na maandalizi ya michezo iliyosalia kabla ya msimu huu 2022/23 haujafikia tamati
Ruvu Shooting inaburuza mkia wa Ligi Kuu Tanzania bara ikiwa na alama 20, ikicheza michezo 27 hadi sasa
"Tutaendelea kujiweka sawa kwa michezo iliyobaki, niaamini wachezaji wangu watapambana hadi mwisho, tulipo sasa sio pazuri lakini hatujakata tamaa," alisema
Mara ya mwisho Ruvu Shooting ilishuka 2014/15 pamoja Polisi Tanzania iliyokuwa ikiburuza mkia kwa alama 25 huku Toto African na African Sports zikipanda Ligi Kuu
Ruvu Shooting ilirejea Ligi Kuu 20l6/17 sambamba na Mbao FC na kumaliza msimu ikiwa nafasi ya saba na alama 36 huku Mbao ikimaliza ya 12 kwa alama 33
Sasa wanaburuza mkia kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama 20 baada ya kucheza mechi 27
Mechi tatu zilizosalia wanahitaji kushinda zote na pengine nafasi ambayo wanaweza kuifikia ni kicheza play-off kwani Mtibwa Sugar inayoshika nafasi ya 12 ambayo ni juu ya play-off ina alama 29 alama ambazo Ruvu Shooting wanaweza kuzifikia kama watashinda mechi zao zilizobaki



