Azam Fc yatimiza masharti CAF, yainunua Baobab Queens

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th June 2023


Azam Fc yatimiza masharti CAF, yainunua Baobab Queens

Klabu ya Azam FC imeingia makubaliano ya kuimiliki Baobab Queens ya Dodoma kwa muda wa mwaka mmoja nili kutimiza sharti la CAF ambao wameagiza klabu zote zitakazoshiriki michuano ya CAF msimu ujao lazima ziwe na timu za Wanawake

Azam kama ilivyokuwa kwa Singida Fountain Gate (zamani Singida BS), zilikata tiketi ya michuano ya kimataifa msimu ujao, lakini zilikuwa zikibanwa na masharti yaliyowekwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) likitaka klabu shiriki zote kulazimika kuwa na timu za soka za wanawake

Singida ilimalizana mapema na Fountain Gate kwa kuuza hisa zao na kubadilisha hadi jina ikiwapa fursa ya kuimiliki timu ya wanawake ya Fountain Gate Princess iliyopo Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) kabla ya Azam nayo kufikia makubaliano maalum na Baobab Queens

Hii hapa taarifa iliyotolewa na Azam Fc;

 "Katika kutekeleza agizo la kikanuni la leseni za vilabu kutoka Shirikisho la Soka barani Afrika, CAF, Azam FC inayo furaha kuutangazia umma kwamba imeingia makubaliano ya ushirikiano na klabu ya soka la wanawake ya Baobab Queens ya Dodoma.

Kwa mujibu wa kanuni mpya za CAF, klabu yoyote itakayopata nafasi ya kushiriki mashindano ya Afrika kuanzia msimu wa 2023/24, itapaswa aidha kuwa na timu ya wanawake au kushirikiana katika uendeshaji na taasisi nyingine yenye timu ya wanawake.

Kwa makubaliano hayo na Baobab, ni rasmi sasa kwamba klabu hiyo ya Dodoma itakuwa klabu dada ya Azam FC kuanzia msimu ujao"


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.