Simba - Local - Transfer

Simba kumalizana na Sawadogo

Joel JJ By Joel JJ
30 Jun 2023
Simba kumalizana na Sawadogo

Uongozi wa Simba umesema wanatumia utaratibu mzuri kulingana na vipengele vya mikataba yao na wachezaji inapofika hatua ya kuachana na mchezaji ambaye bado mkataba wake na klabu upo hai, jambo ambalo pia wanalitekeleza kwa kiungo mkabaji Ismael Sawadogo

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally, baada ya madai kuwa klabu hiyo inashindwa kuachana na Sawadogo kutokana na kuitaka kumlipa Sh. milioni 700 ili kuvunja mkataba wake.

Ahmed amesema mchezaji anaposaini mkataba na Simba kuna makubaliano yanakuwapo mwanzoni ya jinsi ambavyo akishindwa kuendelea kuitumikia klabu hiyo au viongozi wakihitaji kuvunja mkataba wanachotakiwa kukifanya kwanza.

Alisema Sawadogo ana mkataba wa mwaka mmoja na wako kwenye mazungumzo ya kutoendelea naye kwa msimu ujao na baada ya maafikiano ya pande zote mbili wataweka wazi kuachana naye rasmi.

Ahmed alisema Simba inaendeshwa kisasa katika mazungumzo hayo na si suala la fedha kwa sababu kabla ya kusaini mkataba kuna kipengele ambacho kiko wazi mchezaji au klabu atakapovunja mkataba na anapouzwa nini kifanyike kabla.

"Hayo masuala la Sh. milioni 700 sijui yametoka wapi kwa sababu kila kitu kipo wazi, ni kweli Sawadogo hatutaendelea naye kwa msimu ujao na tuko kwenye mazungumzo ya kuvunja mkataba wake," alisema Ahmed

Aliongeza kuwa suala la fedha ya kumlipa mchezaji halijadiliwi bali linakuwapo kwenye mkataba ambao wanaingia naye anaposaini kuitumikia klabu hiyo na hadi sasa hakuna mchezaji ambaye ameachana nao anayedai haki zake.

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
13h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
14h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
16h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
16h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
17h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
17h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
17h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
17h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
18h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
20h ago
READ MORE →