Yanga yaalikwa sherehe za Uhuru Malawi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd July 2023


Yanga yaalikwa sherehe za Uhuru Malawi

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga wamealikwa nchini Malawi kwenye maadhimisho ya sherehe za Uhuru wa nchi hiyo ambazo zitafanyika Julai 06 2023

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema kwa heshima waliyopewa na Malawi, wamelazimika kuwaita wachezaji kambini kwa ajili ya kuhudhuria mwaliko huo wakiongozana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Samia Suluhu Hassan

Kamwe amesema wachezaji 15 wa kikosi cha kwanza wataambatana na wachezaji wengine sita kutoka timu ya vijana

Kamwe amesema mwaliko huo ni matokeo ya mafanikio ambayo Yanga wamepata katika misimu miwili iliyopita

"Tumepokea mwaliko maalumu kutoka kwa Serikali ya Malawi kucheza mchezo maalumu kwenye maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa Malawi itakayofanyika Julai 6, 2023. Hii ni heshima ya kipekee kwa Tanzania na klabu ya Yanga kualikwa kwenye sherehe kubwa ya nchi ambayo itawakutanisha marais wa nchi mbalimbali akiwemo Rais wa Tanzania Mama Samia Sluhu Hassan"

"Mwaliko huu unatosha kuonyesha ukubwa wa klabu yetu na heshima ambayo tunapewa huko nje. Kwa mara nyingine tutakwenda Malawi kwa ndege maalum ambayo itaturudisha nchini baada ya mchezo," alitamba Kamwe

Wachezaji wa Yanga wanatarajia kuripoti kambini siku ya kesho Jumanne na timu kuondoka nchini mapema siku ya Jumatano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.