Winga Elie Mpanzu anahesabu siku tu kabla ya kujiunga na Simba pale dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa mwezi Disemba, imefahamika
Baada ya mvutano wa kimkataba kati yake na AS Vita, Mpanzu sasa ni mchezaji huru baada ya kugomea ofa ya kusaini mkataba mpya kuendelea kuitumikia AS Vita
Alikwenda barani Ulaya kufanya majaribio katika klabu kadhaa lakini hakufanikiwa
Chanzo cha kuaminika kutoka DR Congo, kimethibitisha kuwa Mpanzu atajiunga na Simba
"Mpanzu atakuja huko Tanzania kucheza Simba mwezi Januari. Kulikuwa na shida ya mkataba ndio sababu hakusajiliwa katika dirisha lililopita"
"Lakini kwa sasa ni mchezaji huru, ana makubaliano ya kujiunga na Simba katika dirisha dogo," kilieleza chanzo
Katika dirisha lililopita la usajili, Simba ilifanya jitihada kubwa za kumsajili Mpanzu lakini haikuwezekana baada ya mchezaji huyo kupata mwaliko wa kufanya majaribio Ubelgiji siku chache kabla ya dirisha la usajili kufungwa



