Local,Normal News,Fountain, Singida BS

Ijumaa ni Derby ya Mapacha Singida

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Oct 2024
Ijumaa ni Derby ya Mapacha Singida

Wenyewe wanaiita Pacha Derby! Ni siku ya Ijumaa Oktoba 25 nyasi za uwanja wa CCM Liti mkoani Singida zitawaka moto pale timu 'mapacha' Singida Black Stars na Fountain Gate zitakapoumana

Hii itakuwa mechi ya aina yake ambayo itazikutanisha timu mbili bora katika ligi kuu ya NBC msimu huu

Singida BS iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikikusanya alama 19 baada ya mechi 7 wakati Fountain Gate wako nafasi ya nne wakiwa na alama 16 baada ya mechi 8

Upinzani wa timu hizi ulianza msimu uliopita pale baadhi ya waliokuwa mabosi wa Singida Big Stars kujitoa na kuinunua Ihefu Fc huku wakiondoka na karibu nyota wote wa kigeni waliokuwa wakiitumikia timu hiyo

Baadae Ihefu Fc ikabadili jina na kuitwa Singida Black Stars huku ikihamishia makazi yake Singida

Singida Big Stars ikabadilishwa jina na kuwa Singida Fountain Gate na kuhamishia makazi yake jijini Mwanza yalipokuwa makazi ya wamiliki wapya walioinunua timu hiyo na kuibadili jina kuiita Fountain Gate

Imeitwa Pacha Derby kwa sababu wamiliki wa timu hizi walikuwa pamoja kabla ya sintofahamu iliyojitokeza baada ya Singida Big Stas kuuzwa

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’