Mkurugenzi wa michezo wa Arsenal Edu amechukua uamuzi wa kuondoka katika klabu hiyo mara moja
Edu amekuwa nchini Brazil kwa masuala ya kibinafsi na alirejea Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita
Kulingana na Sky Sports News, Mbrazil huyo amekuwa akihusishwa kujiunga na kundi la vilabu vya Evangelos Marinakis
Evangelos Marinakis kwa sasa inajumuisha klabu za Nottingham Forest, Olympiacos na Rio Ave
Hata hivyo bado haijulikani ikiwa hiyo ndiyo sababu iliyopelekea Edu ajiuzulu ghafla
Edu (42) ana uhusiano mkubwa na mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta, ambaye ameijenga upya Arsenal ambaye kwa pamoja wameshirikiana kuijenga upya Arsenal na kuirejesha katika mbio za kuwania taji la ligi kuu ya Uingereza



