Mkurugenzi wa Michezo Arsenal abwaga manyanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th November 2024


Mkurugenzi wa Michezo Arsenal abwaga manyanga

Mkurugenzi wa michezo wa Arsenal Edu amechukua uamuzi wa kuondoka katika klabu hiyo mara moja

Edu amekuwa nchini Brazil kwa masuala ya kibinafsi na alirejea Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita

Kulingana na Sky Sports News, Mbrazil huyo amekuwa akihusishwa kujiunga na kundi la vilabu vya Evangelos Marinakis

Evangelos Marinakis kwa sasa inajumuisha klabu za Nottingham Forest, Olympiacos na Rio Ave

Hata hivyo bado haijulikani ikiwa hiyo ndiyo sababu iliyopelekea Edu ajiuzulu ghafla

Edu (42) ana uhusiano mkubwa na mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta, ambaye ameijenga upya Arsenal ambaye kwa pamoja wameshirikiana kuijenga upya Arsenal na kuirejesha katika mbio za kuwania taji la ligi kuu ya Uingereza


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.