Wiki mbili baada ya kurejea kutoka kwenye majeraha yaliyomuweka nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi 12, nyota wa Brazil Neymar ameumia paja akiitumikia Al-Hilal kwenye Ligi ya Mabingwa Asia.
Katika dakika ya 58 ya ushindi wa 3-0 wa Al Hilal dhidi ya Esteghlal ya Iran, Neymar aliingia uwanjani lakini hakudumu uwanjani kwa muda mrefu, akatoka tena dakika ya 87 baada ya kwenda chini na kushika nyuma ya mguu wake wa kulia
Mechi dhidi ya Esteghlal ilikuwa mechi ya pili kwa Neymar tangu aliporejea baada ya kupona jeraha la meniscus katika mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia na Brazil dhidi ya Uruguay
Alirejea uwanjani dhidi ya Al Ain mnamo Oktoba 21. Neymar hawezi kucheza katika Ligi Kuu ya Saudia kwa sasa kwa sababu hajasajiliwa
Katika miaka ya hivi karibuni, Neymar ameandamwa na majeraha ya mara kwa mara. Akiwa Paris Saint-Germain alikumbana na majeraha ya aina mbalimbali, ikiwa ni pamoja na jeraha kubwa la metatarsal, lililomweka nje mara nyingi kati ya 2017 na 2023
Msimu uliopita wa kiangazi, alihama kutoka mji mkuu wa Ufaransa hadi Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka miwili na Al-Hilal]
Ada ya uhamisho ilikuwa euro milioni 90. Mnamo 2017, Neymar alijiunga na PSG kutoka FC Barcelona kwa ada ya rekodi ya dunia ya pauni 222 milioni. Kufikia sasa, Mbrazil huyo ameichezea Al Hilal katika mechi saba pekee.



