Mathias Pogba amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kufanya njama za wizi dhidi ya nduguye, Paul Pogba
Mathias Pogba alikamatwa na kushtakiwa kwa njama ya kutaka alipwe fedha ya pauni milioni 11 ($14m) na nyota huyo wa zamani wa Juventus mwishoni mwa 2022 baada ya tukio la utekaji
Sasa, mahakama ya Paris imemkabidhi kakake Pogba kifungo cha miaka mitatu jela, huku miaka miwili ikisimamishwa
Hata hivyo, kijana huyo mwenye umri wa miaka 34 atatumikia kifungo cha mwaka mmoja kilichosalia na bangili ya kielektroniki, badala ya kufungwa jela
Pogba, 31, awali aliwaambia polisi kwamba kundi la marafiki wa utotoni, akiwemo kaka yake mkubwa Mathias, waliomba pesa kwa ajili ya "huduma za ulinzi" - kuanzia miaka 13 nyuma
Pogba mwenyewe alikiri kuwa alifikiria kustaafu mnamo 2023 wakati wa njama hii ya ulaghai lakini sasa amefarijika kufuatia uamuzi huu
Mfaransa huyo ataweza kurejea kwenye soka mwezi Machi 2025 baada ya marufuku yake ya miaka minne ya kutumia dawa za kusisimua misuli kupunguzwa hadi miezi 18 mapema mwaka huu
Kwa sasa ni mchezaji huru baada ya yeye na Juventus kukubaliana kusitisha mkataba wake



