International,Normal News,

Kaka wa Pogba afungwa miaka mitatu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Dec 2024
Kaka wa Pogba afungwa miaka mitatu

Mathias Pogba amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kufanya njama za wizi dhidi ya nduguye, Paul Pogba

Mathias Pogba alikamatwa na kushtakiwa kwa njama ya kutaka alipwe fedha ya pauni milioni 11 ($14m) na nyota huyo wa zamani wa Juventus mwishoni mwa 2022 baada ya tukio la utekaji

Sasa, mahakama ya Paris imemkabidhi kakake Pogba kifungo cha miaka mitatu jela, huku miaka miwili ikisimamishwa

Hata hivyo, kijana huyo mwenye umri wa miaka 34 atatumikia kifungo cha mwaka mmoja kilichosalia na bangili ya kielektroniki, badala ya kufungwa jela

Pogba, 31, awali aliwaambia polisi kwamba kundi la marafiki wa utotoni, akiwemo kaka yake mkubwa Mathias, waliomba pesa kwa ajili ya "huduma za ulinzi" - kuanzia miaka 13 nyuma

Pogba mwenyewe alikiri kuwa alifikiria kustaafu mnamo 2023 wakati wa njama hii ya ulaghai lakini sasa amefarijika kufuatia uamuzi huu

Mfaransa huyo ataweza kurejea kwenye soka mwezi Machi 2025 baada ya marufuku yake ya miaka minne ya kutumia dawa za kusisimua misuli kupunguzwa hadi miezi 18 mapema mwaka huu

Kwa sasa ni mchezaji huru baada ya yeye na Juventus kukubaliana kusitisha mkataba wake

More Stories

Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
4h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
9h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
9h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
11h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
1d ago
READ MORE β†’