Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Singida jana zilitibua mchezo wa kirafiki kati ya Singida BS dhidi ya Yanga uliokuwa ukiendelea katika uwanja wa Airtel
Mchezo huo ulikuwa maalum kuadhimisha uzinduzi wa uwanja huo ambapo Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Hamis Mwinjuma alizindua mapema
Dakika tano tu baada ya kuanza kipindi cha pili, Mwamuzi wa mchezo huo Saadi Mrope alilazimika kusimamisha mchezo baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha
Jonathan Ikangalombo aliitanguliza Yanga kwa bao safi mapema katika kipindi cha kwanza lakini mpira wa faulo uliopigwa na Mauruf Tchakei dakika ya 50 katika kipindi cha pili ulisindikizwa kimiani na upepo na kuisawazishia Singida BS






