Singida BS yazindua uwanja, mvua yatibua

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th March 2025


Singida BS yazindua uwanja, mvua yatibua

Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Singida jana zilitibua mchezo wa kirafiki kati ya Singida BS dhidi ya Yanga uliokuwa ukiendelea katika uwanja wa Airtel

Mchezo huo ulikuwa maalum kuadhimisha uzinduzi wa uwanja huo ambapo Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Hamis Mwinjuma alizindua mapema

Dakika tano tu baada ya kuanza kipindi cha pili, Mwamuzi wa mchezo huo Saadi Mrope alilazimika kusimamisha mchezo baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha

Jonathan Ikangalombo aliitanguliza Yanga kwa bao safi mapema katika kipindi cha kwanza lakini mpira wa faulo uliopigwa na Mauruf Tchakei dakika ya 50 katika kipindi cha pili ulisindikizwa kimiani na upepo na kuisawazishia Singida BS


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.