Local,Normal News,Simba, Stellenbosch

Kocha Simba apania ushindi Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Apr 2025
Kocha Simba apania ushindi Afrika Kusini

Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stellenbosch katika mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC), Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids ameweka mkakati wa kuhakikisha kikosi chake kinashinda mchezo wa mkondo wa pili ugenini na kujihakikishia tiketi ya kucheza fainali

Jumapili, April 27 Simba itakuwa ugenini huko Durban Afrika Kusini kuwania matokeo ya kuwapeleka nusu fainali

Fadlu amesema Simba haitaenda Afrika Kusini kujilinda, bali wanakwenda kusaka ushindi na anaamini watafanikiwa

"Tumeweka msingi, lakini nyumba haijajengwa bado. Tunakwenda kwenye mchezo wa marudiano tukiwa na lengo moja tu kutafuta bao la mapema na kumaliza kazi. Hatutacheza kwa kujilinda. Hatutacheza kwa woga. Hatutaki sare. Tunataka ushindi"

Fadlu amedokeza kuwa katika maandalizi watakayofanya kabla ya safari yao kuelekea Afrika Kusini, watajikita kwenye mipango ya kushambulia kuanzia dakika ya kwanza ili kusaka bao la mapema angalau dakika kumi za kwanza litakalowapa wakati mgumu wenyeji wao.

"Tunajua Stellenbosch ni timu ya vijana wenye kasi, lakini pia wana udhaifu mkubwa wanapowekwa chini ya presha. Wanafungika. Hilo ndilo tunalotaka kulitumia. Hatutaki kuwapa nafasi ya kujipanga. Tunakwenda kuwavamia," alisema Fadlu.

Kimahesabu Simba itahitaji ushindi, sare au kama watapoteza basi sio zaidi ya tofauti ya mabao mawili na zaidi kama watafunga bao la ugenini, watawalazimu wenyeji wao kufunga kuanzia mabao matatu waweze kufuzu

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’