Local,Transfer News,Yanga

Yanga kufanya maboresho makubwa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Apr 2025
Yanga kufanya maboresho makubwa

Uongozi wa Yanga umeweka mkakati wa kuhakikisha msimu ujao wanarejea kwa nguvu kubwa katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Baada ya kucheza fainali ya kombe la Shirikisho 2022/23 na pia kucheza robo fainali ya ligi ya mabingwa 2023/24, msimu huu Wananchi hawakufanikiwa kuvuka hatua ya makundi

Ikiongoza ligi kuu ya NBC ikiwa na alama 70, Yanga tayari imejihakikishia tiketi ya kucheza ligi ya mabingwa msimu ujao

Katika moja ya mahojiano yake, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesikika akitamba kuwa tayari wameanza mchakato wa maboresho ya kikosi ili kuhakikisha msimu ujao wanakuwa bora zaidi hasa katika michuano ya Kimataifa

"Sisi tayari tumejihakikishia tiketi ya kucheza ligi ya mabingwa msimu ujao, Niwaambie tu Wanachama na mashabiki wa Yanga, msimu ujao hatutaki yaliyotokea msimu huu yajirudie"

"Tunataka kufanya vizuri zaidi katika michuano ya ligi ya mabingwa hivyo tutarajie maboresho makubwa ya kikosi chetu," alisema Kamwe

Taarifa za ndani zimedokeza kuwa huenda Yanga ikaongeza wachezaji 6 katika dirisha kubwa litakalofunguliwa mwezi Julai

Maeneo ambayo yanatarajiwa kuwa na maboresho ni safu ya ulinzi hasa mlinzi wa kushoto, kati, kiungo mkabaji, kiungo mshambuliaji na mshambuliaji wa kati

Majina yanayotajwa kuwa kwenye rada ya Yanga ni pamoja na Jonathan Sowah, Feisal Salum, Koimizo Maiga (kiungo mkabaji kutoka Asec) na Agee Basiala Amongo (kiungo mshambuliaji As Maniema Union)

Lakini pia wamo beki Hennock Inonga Baka(FAR Rabat) na kiungo mshambuliaji Arthur Bada kutoka Singida BS ambaye alibadili uraia wake wa Ivory Coast na kuwa Mtanzania

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
43m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’