Local,Normal News,Yanga

Wazee Yanga kuiburuza Bodi ya Ligi Mahakamani

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 May 2025
Wazee Yanga kuiburuza Bodi ya Ligi Mahakamani

Wazee wa klabu ya Yanga wametishia kwenda Mahakamani kuzuia kutangazwa bingwa wa ligi kuu msimu huu kama Yanga haitatendewa haki huku wakiitaka TPLB kutoka hadharani kutaja sababu iliyopelekea kuahirisha mchezo namba 184 kati ya Yanga dhidi ya Simba uliopaswa kupigwa March 08 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano uliowakutanisha wazee wa Yanga uliofanyika Makao Makuu ya klabu, Jangwani, Mzee Msumi amesema watakwenda Mahakamani kuzuia bingwa wa ligi kuu msimu kutangazwa mpaka pale ufafanuzi wa kisheria utakapotolewa na TPLB/TFF

"Hatuwezi kuwaacha watu wachache wanaotaka kuleta vurugu kwa kisingizio kutumia klabu yetu, sisi tutakwenda Mahakamani tukazuie asitangazwe bingwa mpaka ufafanuzi wa kisheria utoke au waje Mahakamani watuthibitishie flani na flani wametoa rushwa au wamefanya hivi"

"Ifahamike kuna watu wametumia gharama kubwa, wametoka mikoani, wametoka nje ya nchi wamekata tiketi ili kushuhudia dabi, sisi tumeamua kuwatetea ili kulinda heshima ya mpira wa Tanzania"

"Hatutajali eti kuna mashindano ya Afcon, kwa sababu hii ni haki yetu ya msingi na tunataka tupate ufafanuzi wa tuhuma zilizotolewa," alisema Mzee Msumi

Wazee wa Yanga wamesisitiza kuwa klabu hiyo sio ya Injinia Hersi Said au Makamu wake Arafat Haji bali ni ya Wanachama wa Yanga

Hivyo wanaunga mkono msimamo wa klabu kutocheza mechi iliyotangazwa na Bodi ya ligi Juni 15 kwa sababu hakuna maelezo yaliyotolewa juu ya kanuni iliyotumika kuahirisha mechi hiyo namba 184

Lakini pia wazee wamesema hawajapata maelezo ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya wale waliotuhumiwa kusababisha mchezo huo kutochezwa

"Moja ya matamko yao (klabu ya Simba), walitangaza wao hawatacheza mechi yoyote mpaka wale waliohusika kuwazuia kufanya mazoezi wachukuliwe hatua, lakini hakuna chochote kilichofanyika zaidi ya kutangazwa tarehe nyingine"

"Hatujui nani aliahirisha mechi, hatujui kanuni gani ilitumika kuahirisha mechi na hatujui ni hatua gani wale waliohusika wamechukuliwa"

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’