Mashabiki wa soka nchini Tanzania na hasa visiwani Zanzibar wanatarajiwa kushuhudia mtanange wa kusisimua wa fainali ya Kombe la CRDB kati ya mabingwa watetezi Yanga SC dhidi ya Singida Black Stars. Mchezo huu wa kuamua bingwa wa msimu huu umepangwa kuchezwa tarehe 28 Juni katika dimba la kisasa la New Amaan Complex, Zanzibar.



