Klabu ya Kaizer Chiefs inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini, imekuwa ikihusishwa na nyota wawili wa Simba Kibu Denis na Jean Charles Ahoua
Hivi karibuni Kocha Mkuu wa timu hiyo Nasreddine Nabi alikuwa Tanzania ambapo alishuhudia mchezo wa ligi kuu kati ya Simba dhidi ya Singida Black Stars uliopigwa uwanja wa KMC Complex Simba ikiibuka na ushindi wa bao 1-0
Inaelezwa Nabi alikuja nchini kwa lengo maalum la kuwafuatilia nyota hao ambapo Chiefs wameshawasilisha yao ya kwanza kwa ajili ya Kibu lakini imekataliwa na Simba
Ofa iliyokataliwa na Simba inakadiriwa kuwa zaidi ya Tsh Milioni 500 taarifa za ndani zikibainisha kuwa Simba haina mpango wa kumuachia Kibu (24) katika dirisha hili
Bado Chief haijawasilisha ofa yoyote kwa ajili ya Ahoua ingawa yawezekana miamba hao wa soka la Afrika Kusini watajaribu kumsajili
Kibu alisaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Simba mwanzoni mwa msimu huu hivyo bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Wekundu hao wa Msimbazi huku Ahoua akiwa bado na mkataba wa miaka miwili



