Local,Transfer News,Yanga, Simba, Azam

Azam Fc yaanza kujipanga na maisha bila Fei Toto

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Jun 2025
Azam Fc yaanza kujipanga na maisha bila Fei Toto

Klabu ya Azam FC imeanza rasmi harakati za kuhakikisha haitingishwi na uwezekano wa kuondokewa na Feisal Salum 'Fei Toto', kiungo wake tegemezi ambaye kwa sasa yupo katika rada za klabu kubwa kama Simba, Yanga, na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.

Ingawa Azam haijaweka wazi hatma ya kiungo huyo, tafsiri ya kiufundi ni wazi klabu hiyo ipo kwenye maandalizi ya mapema kufidia nafasi ya Fei Toto endapo ataondoka msimu ujao.

Azam tayari wamesisitiza kuwa mchezaji huyo hatauziwa chini ya Sh1 bilioni, licha ya kuwa bado na mkataba wa mwaka mmoja.

Katika mchakato huo, Allan Okello, kiungo mshambuliaji wa Vipers mwenye uwezo mkubwa wa kutumia mguu wa kushoto, ndiye anayeonekana kuwa chaguo la kwanza.

Okello si jina geni katika soko la usajili Afrika Mashariki; klabu ya Simba pia iliwahi kumuwinda katika dirisha dogo la usajili lililofunguliwa Desemba 15 mwaka jana, lakini iligonga mwamba kutokana na msimamo mkali wa Rais wa Vipers, Lawrence Mulindwa, ambaye huwa hana urahisi wa kuuza nyota wake muhimu.

Kwa msimu huu pekee, Okello ameonyesha kiwango cha juu akifunga mabao 19, akiwa katika msimu wake wa pili tangu arudi Vipers.

Klabu hiyo pia inaongoza Ligi Kuu ya Uganda baada ya mechi 30, ikiwa imeshinda 21, sare 6 na kupoteza 3 rekodi inayoonyesha mchango mkubwa wa Okello.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’