Uongozi wa Simba umepitisha mlinda lango namba moja wa timu hiyo Moussa Camara aendelee kulinda lango la wekundu hao wa Msimbazi kwa msimu mwingine, imefahamika
Camara alitua Simba msimu uliopita akitokea Horoya Ac ya Guinea, alisaini mkataba wa mwaka mmoja uliokuwa na kipengele cha kuongeza mwaka wa pili kama uongozi utaridhishwa na uwezo wake
Taarifa kutoka ndani ya uongozi imethibitisha kuwa baada ya majadiliano ya muda, mwafaka umefikiwa na golikipa bora huyo wa ligi kuu msimu uliopita, ataendelea kuitumikia Simba
Sasa Simba inapambana kukamilisha usajili wa mlinda lango mwingine Yacoub Mohammed kutoka klabu ya JKT Tanzania
Tayari Simba imeachana na magolikipa wawili Aishi Manula na Hussein Abel ambao mikataba yao imemalizika



