Uongozi wa Simba umepitisha mlinda lango namba moja wa timu hiyo Moussa Camara aendelee kulinda lango la wekundu hao wa Msimbazi kwa msimu mwingine, imefahamika
Camara alitua Simba msimu uliopita akitokea Horoya Ac ya Guinea, alisaini mkataba wa mwaka mmoja uliokuwa na kipengele cha kuongeza mwaka wa pili kama uongozi utaridhishwa na uwezo wake





