Wakati akizungumza na wanahabari jana, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alitoa 'code' ya kocha ambaye Yanga wamemuajiri kukiongoza kikosi cha mabingwa hao wa kihistoria katika msimu ujao
Kamwe alidokeza kuwa kocha huyo ni kijana na mwenye kiu ya mafanikio. Ni kocha ambaye anaendana na mahitaji ya Yanga yenye malengo ya kulisaka taji la Afrika





