Local,Transfer News,Simba, Singida

Ateba kumpisha Sowah Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jul 2025
Ateba kumpisha Sowah Simba

Klabu ya Simba SC huenda ikafanya maamuzi magumu kuhusu hatma ya mshambuliaji wao raia wa Cameroon, Lionel Ateba, kufuatia usajili mpya wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka Ghana, Jonathan Sowah, aliyesajiliwa kutoka klabu ya Singida Black Stars.

Usajili wa Sowah, ambaye alifunga mabao 13 katika mechi 14 pekee msimu uliopita akiwa na Singida BS, unaifanya Simba kuwa na washambuliaji watatu wa kigeni: Jonathan Sowah, Steven Mukwala na Lionel Ateba.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu, Maghreb Fez ya Morocco tayari imetuma ofa rasmi kwa ajili ya kumsajili Ateba, na Simba huenda ikaisikiliza kwa ofa hiyo kama sehemu ya kupanga upya safu yake ya ushambuliaji.

Inaelezwa kuwa Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, ameshathibitisha kumuhitaji Steven Mukwala kama sehemu muhimu ya mipango yake kwa msimu ujao. Mukwala, ambaye pia alifunga mabao 13 msimu uliopita, alimaliza msimu akiwa na kiwango bora Simba ikipuuzia ofa zote zilizowasilishwa kwa ajili yake.

Kwa upande mwingine, Lionel Ateba, licha ya kuwa na msimu mzuri akipachika mabao 13, anaonekana kuwa kwenye nafasi ya kupisha ujio wa Sowah.

Ushindani mkali unaotarajiwa kwenye eneo la ushambuliaji unaweza kumlazimu Mcamerooni huyo kutafuta nafasi ya kucheza zaidi nje ya Msimbazi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’