Local,Normal News,Simba

Nyota wapya Simba waongeza mzuka Ismailia

Joel JJ By Joel JJ
4 Aug 2025
Nyota wapya Simba waongeza mzuka Ismailia

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids jana alipokea kundi la pili la wachezaji 11 wa timu hiyo waliowasili Ismailia huko Misri kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2025/26

Wachezaji hao wameungana na kundi la kwanza lililotua Misri tangu Jumatano iliyopita leo wakiingia siku ya tano ya maandalizi

Kuongezeka kwa wachezaji hao kutaongeza mzuka katika kambi hiyo, kutokana na wachezaji watazidi kuongeza idadi kufuatia awali kuwa na wachezaji wachache.

Nyota wapya walioingia kambini jana ni pamoja na kiungo Alassane Kante, winga Mohamed Bajaber na mshambuliaji Jonathan Sowah

Wengine ni Hussein Semfuko, Morice Abraham na pia wamo Bashir Salum, Ally Mbegu na Alex Erasto kutoka timu ya vijana ya Simba (U20)

Simba itakuwa kambini kwa wiki nne kujiandaa kwa msimu mpya, ambapo inarudi Ismailia kwa mara ya pili kama ambavyo ilifanya msimu uliopita.

Wachezaji wengine ambao hawajajiunga na kambi hiyo ni pamoja na wale wanaoshiriki Fainali za Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN walioko kikosi cha Taifa Stars na kiungo  Neo Maema ambaye yuko katika kikosi cha Afrika Kusini

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →