Ateba amekwama Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th August 2025


Ateba amekwama Simba

Klabu ya Simba imefikia makubalino ya kuachana na mshambuliaji Lionel Ateba, imefahamika

Ateba aliyetua Simba msimu uliopita akitokea klabu ya USM Alger, anaondoka Msimbazi baada ya kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi kwa msimu mmoja akifunga mabao 13 kwenye ligi

Baada ya kukamilisha usajili wa kiungo kiraka Naby Camara, Simba ililazimika kupunguza nyota mmoja wa kigeni

Lilikuwa ni suala la muda tu kwa maamuzi hayo kufikiwa pale Simba ilipomsajili Jonathan Sowah kutoka Singida BS na kuwa na washambuliaji watatu wa kigeni

Baada ya Ateba kuondoka, nyota wa kigeni ambao wako katika kikosi cha Simba ni Moussa Camara, Rushine De Reuck, Chamou Carabou, Alassane Kante, Mohamed Bajaber na Neo Maema

Wengine ni Joshua Mutale, Jonathan Sowah, Jean Charles Ahoua, Elie Mpanzu, Steven Mukwala na Naby Camara

Dirisha la usajili la michuano ya ligi ya mabingwa limefungwa usiku wa kuamkia leo August 16


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.