Fadlu atimka Simba, mbadala wake ni suala la muda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd September 2025


Fadlu atimka Simba, mbadala wake ni suala la muda

Ni suala la muda klabu ya Simba itatangaza kuachana na kocha Fadlu Davids baada ya makubaliano ya pande mbili kufikiwa

Fadlu juzi aliiongoza Simba kwa mara ya mwisho katika mchezo wa hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United, mchezo ambao Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 ugenini

Tayari Simba imeanza mchakato wa kumsaka mrithi wake haraka ili aendelee na majukumu akishirikiana na kocha Selemani Matola

Fadlu yuko mbioni kujiunga na klabu ya Raja Casablanca ambapo inaelezwa ameondoka na wasaidizi wawili aliokuwa nao Simba, Darian Wilker na Wayne Sandilands

Miongoni mwa majina ya makocha wanaotajwa Msimbazi ni pamoja na mkufunzi wa timu ya Taifa ya Kenya Benny Mccarthy huku pia jina la Miguel Gamondi mkufunzi wa Singida Black Stars likitajwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.