Mtihani wa kwanza kwa Pantev Eswatini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th October 2025


Mtihani wa kwanza kwa Pantev Eswatini

Baada ya kutua Eswatini jana, kikosi cha Simba leo kitaanza maandalizi yake nchini humo kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika (CAFCL) dhidi ya Nsingizini Hotspurs

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa keshokutwa Jumapili, Oktoba 19 nchini humo

Meneja Mkuu wa Dimitar Pantev atakuwa na siku mbili za kukiandaa kikosi chake kabla ya kuwavaa Nsingizini katika mchezo ambao Simba inahitaji ushindi ili kurahisisha kazi kwenye mechi ya marudiano ambayo itapigwa wiki ijayo Oktoba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema wachezaji wote ambao wamesafiri na timu hiyo Eswatini wako katika hali nzuri na leo watafanya mazoezi yao ya kwanza nchini humo

Hii itakuwa mechi rasmi ya kwanza ya mashindano kwa Pantev ambaye alijiunga na Simba akitokea klabu ya Gaborone United ya Botswana aliyoiongoza hatua ya awali ya ligi ya mabingwa msiimu huu na kuondoshwa na Simba

Dakika 180 za mechi kati ya Simba dhidi ya Gaborone United, zilitosha kuwashawishi mabosi wa Simba kumuajiri kocha huyo raia wa Bulgaria ambaye aliwapa Gaborone United ubingwa wa ligi kuu msimu uliopita

Jukumu lake la kwanza sasa ni kuivusha Simba hatua ya makundi ya CAFCL msimu huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.