Baada ya kutua Eswatini jana, kikosi cha Simba leo kitaanza maandalizi yake nchini humo kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika (CAFCL) dhidi ya Nsingizini Hotspurs
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa keshokutwa Jumapili, Oktoba 19 nchini humo
Meneja Mkuu wa Dimitar Pantev atakuwa na siku mbili za kukiandaa kikosi chake kabla ya kuwavaa Nsingizini katika mchezo ambao Simba inahitaji ushindi ili kurahisisha kazi kwenye mechi ya marudiano ambayo itapigwa wiki ijayo Oktoba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema wachezaji wote ambao wamesafiri na timu hiyo Eswatini wako katika hali nzuri na leo watafanya mazoezi yao ya kwanza nchini humo
Hii itakuwa mechi rasmi ya kwanza ya mashindano kwa Pantev ambaye alijiunga na Simba akitokea klabu ya Gaborone United ya Botswana aliyoiongoza hatua ya awali ya ligi ya mabingwa msiimu huu na kuondoshwa na Simba
Dakika 180 za mechi kati ya Simba dhidi ya Gaborone United, zilitosha kuwashawishi mabosi wa Simba kumuajiri kocha huyo raia wa Bulgaria ambaye aliwapa Gaborone United ubingwa wa ligi kuu msimu uliopita
Jukumu lake la kwanza sasa ni kuivusha Simba hatua ya makundi ya CAFCL msimu huu



