Kiungo mshambuliaji wa Yanga Offen Chikola anatarajiwa kujiunga na klabu ya Singida Black Stars kwa mkopo.
Baada ya mwanzo wa kusuasua kwenye kikosi cha Yanga, nyota huyo ametolewa kwa mkopo ili apate muda zaidi wa kucheza.
Anakuwa mchezaji wa pili wa ndani kutolewa kwa mkopo na Yanga kwenye dirisha hili baada ya Denis Nkane aliyetua TRA United.
Nyota wa kigeni ambao nao wanatajwa kutolewa kwa mkopo na Yanga ni Mohamed Doumbia na Ecua Celestin aliyetua JS Kabylie ya Algeria



