Chikola kutua Singida BS kwa mkopo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th January 2026


Chikola kutua Singida BS kwa mkopo

Kiungo mshambuliaji wa Yanga Offen Chikola anatarajiwa kujiunga na klabu ya Singida Black Stars kwa mkopo.

Baada ya mwanzo wa kusuasua kwenye kikosi cha Yanga, nyota huyo ametolewa kwa mkopo ili apate muda zaidi wa kucheza.

Anakuwa mchezaji wa pili wa ndani kutolewa kwa mkopo na Yanga kwenye dirisha hili baada ya Denis Nkane aliyetua TRA United.

Nyota wa kigeni ambao nao wanatajwa kutolewa kwa mkopo na Yanga ni Mohamed Doumbia na Ecua Celestin aliyetua JS Kabylie ya Algeria


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.