Local,Normal News,Yanga

Mzize ndio basi tena msimu huu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Mar 2026
Mzize ndio basi tena msimu huu

Mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize amekamilisha matibabu yake nchini Afrika Kusini akitarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi minne.

Baada ya kuandamwa na mfululizo wa majeraha, uongozi wa Yanga umechukua hatua ya kuhakikisha nyota huyo anapata matibabu sahihi na kupata muda mrefu wa kuponya jeraha lake kabla ya kurudi tena uwanjani.

Mzize aliumia mwanzoni mwa msimu Septemba 27, 2025, katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete Benguela ya Angola na kuanza mchakato mrefu wa matibabu pamoja na upasuaji wa Desemba 2025, kabla ya kurudi tena kikosini.

Baada ya kurejea mshindi huyo wa tuzo ya Bao Bora la Mwaka 2025 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), alijitonesha wakati wa maandalizi ya mechi ya mwisho ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya dhidi ya JS Kabylie.

Kwa mujibu wa daktari wa klabu ya Yanga, Moses Etutu, Mzize atakuwa nje ya uwanja hadi kufikia mwisho wa msimu huu na hivyo kutarajiwa kurudi kucheza tena katika msimu ujao wa mashindano

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’