Mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize amekamilisha matibabu yake nchini Afrika Kusini akitarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi minne.
Baada ya kuandamwa na mfululizo wa majeraha, uongozi wa Yanga umechukua hatua ya kuhakikisha nyota huyo anapata matibabu sahihi na kupata muda mrefu wa kuponya jeraha lake kabla ya kurudi tena uwanjani.





