Tulishakodi ndege kuelekea Tabora - Kamwe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th March 2026


Tulishakodi ndege kuelekea Tabora - Kamwe

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema klabu ilishafanya utaratibu wa kukodi ndege binafsi kuelekea mkoani Tabora kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons kabla ya mabadiliko yaliyotangazwa na Bodi ya ligi jana kuwa mchezo huo utapigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Kamwe amesema mpaka jana walikuwa wamejiandaa na safari ya kuelekea Tabora leo, lakini baada ya maelekezo ya Bodi ya ligi, safari hiyo sasa imeelekea Dodoma.

"Tumepokea barua kutoka Bodi ya ligi jana kuwa mechi itachezwa Dodoma. Kabla ya hapo tulivyoona Tanzania Prisons wanafanya maandalizi ya mechi kupigwa Tabora sisi tuliwasiliana na Shirika moja la ndege na tukaweka 'booking' ya ndege ya kutupeleka Tabora."

"Sisi kama klabu tulikuwa hatuna shida yoyote kuelekea Tabora tuliangalia ni utaratibu gani unaweza kutufikisha Tabora haraka kwani kiuhalisia isingekuwa rahisi kusafiri kwa basi na treni ilikuwa imejaa."

"Tulichokuwa tunasubiri ni taarifa kutoka Bodi ya ligi kama wangetuambia mchezo ni Tabora leo hii tungeondoka hapa kuelekea Tabora kwani taratibu zote za safari zilikuwa zimekamilika," alisema Kamwe.

Yanga imeondoka jijini Dar es salaam mapema leo wakielekea Dodoma huku wapinzani wao Tanzania Prisons ambao tayari walikuwa wamefika Tabora, wanalazimika kuelekea mkoani Dodoma


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.