Local,Normal News,

Simba yaunguma Singida, yaichapa Singida BS 2-1

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Mar 2026
Simba yaunguma Singida, yaichapa Singida BS 2-1

Simba imetakata uwanja wa Airtel huko Singida ikiibuka ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida BS katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Ulikuwa mchezo mgumu lakini Simba imetumia uzoefu wake kuchomoza na ushindi huo muhimu ugenini.

Mapema tu dakika ya 7 Anicet Oura alifungua akaunti yake ya mabao kwenye ligi akiifungia Simba bao muhimu baada ya walinzi wa Singida BS kuzembea kuondoa hatari langoni kwao.

Hata hivyo Singida BS walirejea mchezoni dakika chache kabla ya mapumziko Mossi akifunga bao la kichwa akimalizia krosi ya Lamine Jarjou.

Kipindi cha pili ni Singida iliyokuwa ikionekana hatari kupitia mashambulizi ya kushitukiza na katka matukio mawili wachezaji wao Khalid Aucho na Joseph Guede walionekana kama kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari lakini matukio hayo hayakumshawishi mwamuzi wa mchezo huo kutoa mkwaju wa penati.

Alikuwa 'super sub' Elie Mpanzu aliyepeleka kilio Singida BS akifunga bao la ushindi dakika ya 85 akimalizia krosi ya Clatous Chama baada ya kuwazidi mbio walinzi wa Singida BS waliokuwa wakidhani ameotea.

Ni alama tatu muhimu kwa Simba ambazo zinawafanya wasogee kwenye nafasi ya tatu katika msimamo wakifikisha alama 27.

Mapema TRA United iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo Fc katika mchezo uliopigwa uwanja wa Black Rhino, Manyara.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’