Local,Normal News,Simba, Azam

Barker aweka mkakati wa kuvuna alama tatu dhidi ya Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Apr 2026
Barker aweka mkakati wa kuvuna alama tatu dhidi ya Azam Fc

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amesema anatambua mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Azam Complex utakuwa mgumu lakini wamejiandaa vyema kusaka matokeo ya ushindi.

Akizungumza katika mkutano na wanahabari mapema leo, Barker amesema Azam Fc ni timu ngumu kufungika, takwimu zao za kutopoteza mchezo pamoja na kuruhusu mabao machache ni ishara ya uimara wao.

Barker amesema ni mchezo ambao hatarajii kuwa na nafasi nyingi lakini jambo muhimu kwa vijana wake ni kutumia vyema nafasi watakazopata.

"Nafikiri timu zote ni bora Azam Fc wameruhusu mabao machache kama ivyo kwetu hivyo itakuwa mechi ambayo itaamuliwa na mambo madogo"

"Sitarajii kuwa mchezo wenye nafasi nyingi kwa kila timu lakini jambo muhimu kwetu ni kutumia vyema kila nafasi tutakayopata"

"Natambua Azam Fc ni timu ngumu kufungika, hawajapoteza mchezo kwenye ligi hivyo lazima tuwe katika kiwango bora na ufanisi kuweza kupata ushindi"

"Tunatengeneza nafasi nyingi, naamini tutaendelea na mwendo huo, muhimu ni kuhakikisha tunazitumia nafasi hizo," alisema Barker.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
15h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
18h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
18h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
20h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’