International,Normal News,Manchester United, Local

Rooney ampigia chapuo Carrick akabidhiwe mikoba Man United

Joel JJ By Joel JJ
8 May 2026
Rooney ampigia chapuo Carrick akabidhiwe mikoba Man United

Nguli wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney, ameendelea kusisitiza kuwa Michael Carrick anastahili kupewa nafasi ya kudumu ya kuinoa klabu hiyo kufuatia matokeo mazuri aliyoyapata tangu alipopewa jukumu la kuinoa timu hiyo kwa muda.

Rooney amesema Carrick ameonyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi kwa kuirejesha Manchester United kwenye ushindani ndani ya muda mfupi, huku akieleza kuwa mafanikio yake hayapewi uzito unaostahili kwa sababu ni kocha mchanga na raia wa Uingereza.

“Kama Manchester United wangemleta Luis Enrique au Thomas Tuchel na wakashinda michezo 10 kati ya 14 mfululizo, kila mtu angesema jambo la ajabu na kumsifia kwa kila aina ya sifa. Michael Carrick kafanya hivyo na hakuna anayemsifia kwa sababu ni kocha mchanga na ni Muingereza anapuuzwa,” alisema Rooney.

Rooney ambaye aliwahi kucheza pamoja na Carrick kwa mafanikio makubwa ndani ya Manchester United, amesema kocha huyo anaifahamu vyema DNA ya klabu hiyo na ana uwezo wa kuiongoza kwa muda mrefu.

“Michael Carrick ni mtu mwelevu sana, ni kocha mzuri sana na nadhani anaweza kuiongoza timu kwa muda mrefu tu. Tangu timu iwe chini yake Manchester United imepata utulivu na mashabiki sasa wanafurahia matokeo.”

Tangu apewe jukumu la kuiongoza timu hiyo mapema mwaka huu baada ya kuondoka kwa kocha wa zamani, Carrick ameiongoza United kushinda michezo 10 kati ya 14 kwenye ligi, rekodi iliyowafanya wengi kuanza kumtaja kama chaguo sahihi la kudumu Old Trafford.

Chini ya Carrick, Manchester United imefanikiwa kupata ushindi dhidi ya vigogo kama Manchester City, Liverpool FC, Chelsea FC na Arsenal FC, huku ikipewa nafasi kubwa ya kumaliza ndani ya nne bora na kurejea kwenye michuano ya UEFA Champions League msimu ujao.

Katika mahojiano tofauti, Carrick mwenyewe amesisitiza kuwa bado ameweka akili yake kwenye kuisaidia timu kumaliza msimu vizuri licha ya mjadala mkubwa unaoendelea kuhusu hatma yake ndani ya klabu hiyo.

Mashabiki wengi wa Manchester United wameonekana kumuunga mkono Carrick kutokana na mabadiliko ya haraka ya kiwango cha timu, huku baadhi wakiamini kuwa kurejesha utambulisho wa klabu hiyo kunahitaji mtu anayeifahamu vizuri historia na tamaduni za United kama Carrick.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →