Tchouamni, Valverde wapigwa faini ya kihistoria Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ • 8th May 2026


Tchouamni, Valverde wapigwa faini ya kihistoria Real Madrid

Klabu ya Real Madrid imewachukulia hatua kali viungo Aurélien Tchouaméni na Federico “Fede” Valverde kwa kuwatoza faini ya Euro 500,000 kila mmoja, sawa na zaidi ya Sh1.5 bilioni za Tanzania, kufuatia tukio la kinidhamu lililotokea ndani ya klabu hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada ya wawili hao kuingia kwenye mzozo mkubwa uliotajwa kuzua taharuki ndani ya kikosi cha Real Madrid wakati wa mazoezi katika kituo cha Valdebebas, jijini Madrid.

Kwa mujibu wa taarifa, ugomvi huo ulianzia mazoezini baada ya kuchezeana faulo kali kabla ya kuendelea hadi kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

Ripoti hizo zinaeleza kuwa hali ilihitaji viongozi wa benchi la ufundi pamoja na baadhi ya wachezaji kuingilia kati ili kutuliza vurugu hizo.

Licha ya uzito wa tukio hilo, Real Madrid imeamua kutowasimamisha nyota hao kucheza mechi zijazo baada ya wote wawili kuwasilisha maombi rasmi ya radhi kwa viongozi wa klabu, benchi la ufundi pamoja na wachezaji wenzao.

Chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo kimeeleza kuwa uongozi wa Madrid umechukua hatua hiyo kama sehemu ya kulinda nidhamu na heshima ya klabu.

“Hakuna mchezaji aliye juu ya sheria ndani ya Real Madrid. Nidhamu ni msingi wa mafanikio ya klabu hii,” kilieleza chanzo hicho.

Faini hiyo inatajwa kuwa miongoni mwa adhabu kubwa zaidi za kifedha kuwahi kutolewa ndani ya klabu hiyo kwa kosa la kinidhamu.

Tukio hilo limezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa soka duniani, huku baadhi wakisifu uamuzi wa klabu kuchukua hatua kali, wakati wengine wakishangazwa na uamuzi wa kutowasimamisha kucheza.

Hata hivyo, viongozi wa Real Madrid wanaamini suala hilo limefungwa rasmi baada ya wachezaji hao kuonyesha majuto na kuahidi kutorudia kosa hilo.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →